RAIS DK.SHEIN ATEMBELEA MRADI UJENZI WA NYUMBA ZA KISASA FUMBA.
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Kampuni ya Azam Group Bw.Said Salim Bakhresa alipotembelea Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za kisasa huko Fumba wilaya ya Magharibi,Mkoa wa Mjini Magharibi leo alipofanya ziara maalum kuangalia ujenzi wa nyumba hizo zinazojengwa na Kampuni ya Azam Group,(kulia ) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibu Nd,Ayoub Mohamed Mahmoud.
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akifuatana na Mwenyekiti wa Kampuni ya Azam Group Bw.Said Salim Bakhresa (kushoto) pamoja na Viongozi mbali mbali wa Serikali wakati alipotembelea Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za kisasa huko Fumba wilaya ya Magharibi,Mkoa wa Mjini Magharibi leo alipofanya ziara maalum kuangalia ujenzi wa nyumba hizo zinazojengwa na Kampuni ya Azam Group,(wa tatu kushoto) Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA) Salum Nassor Khamis,akifuatiwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt.Khalid Salum Mohamed.
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akipanda ngazi ya moja ya nyumba zinazojengwa na Kampuni ya Ujenzi ya Azam Groupakifuatana na Mwenyekiti wa Kampuni hiyo Bw.Said Salim Bakhresa wakati alipotembelea Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za kisasa huko Fumba wilaya ya Magharibi,Mkoa wa Mjini Magharibi leo alipofanya ziara maalum kuangalia ujenzi wa nyumba hizo.
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Mtaalam wa mashine za kutengenezea lami katika Kampuni ya Ujenzi ya Azam Group N.P.Singh (wa pili kulia) wakati alipotembelea Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za kisasa huko Fumba wilaya ya Magharibi,Mkoa wa Mjini Magharibi leo alipofanya ziara maalum,(katikati) Mwenyekiti wa Kampuni ya Azam Group Bw.Said Salim Bakhresa na (kushoto)Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA) Salum Nassor Khamis.
Rais wa Zanzinbar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Kampuni ya Azam Group Bw.Said Salim Bakhresa(kulia) wakati alipotembelea Mtambo wa kutengenezea lami katika Kampuni ya Ujenzi ya Azam Group leo wakati alipotembelea Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za kisasa huko Fumba wilaya ya Magharibi,Mkoa wa Mjini Magharibi (wa pili kulia) Mtaam wa Mtambo N.P.Singh. Picha na Ikulu.
Na Rajab Mkasaba, Ikulu
Zanzibar
RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema kuwa Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar Awamu ya Saba imedhamiria kwa makusudi kuitilia mkazo
na kuiimarisha sekta ya uwekezaji ambayo matunda yake yatawasaidia wananchi wote
wa Zanzibar.
Dk. Shein aliyasema hayo leo
alipofanya mahojiano na waaandishi wa habari kutoka vyombo mbali mbali mara
baada ya kumaliza ziara yake ya kuitembelea miradi ya Kampuni ya Bakhresa
ikiwemo ujenzi wa nyumba huko Fumba pamoja na ujenzi wa hoteli ya kisasa huko
Mtoni mjini Zanzibar.
Dk. Shein alisema kuwa mradi
mkubwa wa ujenzi wa nyumba za kisasa huko Fumba utasaidia kwa kiasi kikubwa
kutokana na Serikali kuweza kupata pato sambamba na wananchi wa Fumba na maeneo
jirani kuweza kupata ajira.
“Fumba ilikuwa imefumba
lakini hivi sasa itafumbuka kwani kukamilika kwa mradi huu Fumba itakuwa ni
sehemu ya pekee katika kukuza uchumi wetu pamoja na kuwasaidia wananchi wote
kutokana na pato litakalopatikana katika maradi huo”,alisema Dk. Shein.
Alisema kuwa matarajio ya
ujenzi huo ambao kwa maelezo ya uongozi wa Kampuni hiyo, eneo hilo litakuwa ni
Dubai ya Zanzibar linatoa matumaini makubwa katika kuuimarisha uchumi wa
Zanzibar, ambapo mradi huo utajulikana kwa jina la ‘Uptown Living’.
Aidha, Dk. Shein alieleza
kuwa nchi nyingi duniani ziliazia na miradi kama hiyo ambazo zilikuwa ni
masikini kuliko Zanzibar lakini hivi sasa zimeweza kupiga hatua kubwa na kuwa
nchi tajiri kutokana na kuwepo miradi kama hiyo na kueleza kuwa kinachofanywa
na serikali katika suala zima la uwekezaji ni tija kwa wananchi wote,
Kutokana na juhudi hizo Dk.
Shein alitoa wito kwa wananchi wa Zanzibar kuheshimu na kufuata taratibu zote
zilizowekwa na Serikali juu ya suala zima la matumizi ya ardhi.
Katika maelezo yake Dk.
Shein alisikitishwa na tabia ya baadhi ya wananchi kuvunja sheria na taratibu
zilizowekwa juu ya umili wa ardhi huku wakitambua kuwa ardhi ni mali ya
serikali hivyo kila mmoja ana jukumu la kuilinda na kuitunza ardhi iliopo.
Kwa upande changamoto ya
ajira kwa vijana wa Zanzibar hasa katika sekta ya utalii, Dk. Shein alieleza
kuwa jambo muhimu ambalo litawapa vijana wa Zanzibar kuajiriwa kwa haraka
katika sekta hiyo ni kuwa na elimu ya fani hiyo.
Alisema kuwa suala la elimu
ni muhimu sana na kutoa wito kwa vijana wa Zanzibar kujikita zaidi katika
kujitafuatia elimu na ndio maana Serikali anayoiongoza imeweza kutilia mkazo
suala hilo kwa kukiimarisha Chuo chake cha Huduma za Watalii kiliopo Maruhubi
kwa kutoa mafunzo ya Cheti, Diploma huku kukiwa na mchakato wa kukiingiza kuwa
ni sehemu ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA).
Dk. Shein alisisitiza kuwa
iwapo vijana watakuwa na elimu ya kutosha suala la upendeleo halitochukua
nafasi huku akitoa inzari umuhimu wa elimu kwa hi sasa kwa vijana hao hasa
katika ushindani wa ajira katika soko la Afrika Mashariki.
Mapema Dk. Shein alipata
nafasi kutembelea mradi ya nyumba za kisasa zinazojengwa na Kampuni ya Bakhresa
huko Fumba akiwa na mwenyeji wake Said Salim Bakhresa na kupata maelezo juu ya
uendelezaji wa mradi huo utakaojenwga nyumba 600 ambapo awamu ya kwanza ni wa
nyumba 92 za kisasa zinazoendelea kujengwa ambazo zitakuwa kwa ajili ya
wananchi wenye kipato cha juu na kipato
cha kati.
Mradi huo ambao mbali ya
nyumba utakuwa na eneo maalum la bustani kwa ajili ya wananchi, bandari ambayo
itawasafirisha wakaazi wa eneo hilo kutoka eneo hilo hadi Dar-es-Salaa kwa boti
maalum zitakazokuwepo eneo hilo huku uongozi huo ukieleza hatua
zitakazochukuliwa katika kuhakikisha suala ziama la ulinzi na usalama
linaimarishwa.
Pia, Dk. Shein alipata fursa
ya kuangalia mtambo wa kisasa wa kupikia lami unaomilikiwa na Kampuni hiyo ya
Bakhresa na baadae kukagua barabara itakayotoka eneo hilo hadi uwanja wa ndege.
Ziara ya Dk. Shein
ilimalizia huko Mtoni nje kidogo ya mji wa Zanzibar ambapo alijionea ujenzi wa
hoteli hiyo itakayokuwa na sifa ya kimazingira ‘Eco Friend’ ambayo inajengwa
kwa umiliki wa Kampuni hiyo ambayo inatarajiwa itakuwa ni ya pekee katika
ukanda wa Afrika Mashariki.
Kwa mujibu wa maelezo ya
Mkuu wa ujenzi wa mradi huo Salim Aziz, alisema kuwa hoteli hiyo itajitosheleza
kwa huduma za maji na umeme na kupunguza
gharama katika matumizi hayo.
Sambamba na hayo, Dk. Shein
alitembela eneo la bahari kuona shughuli za ufukiaji bahari ‘Land Reclamation’
lenye ukubwa wa heka 4 ambalo ni eneo la hoteli hiyo linalotarajiwa kuwa na
maegesho ya meli ndogo na meli kubwa, huduma za bustani ya maji ambayo
inajumuisha michezo ya kila aina itakayochezwa na wananchi pamoja na watalii.
Akimalizia Ziara yake, Dk.
Shein alitembelea Gofu la Mtoni ‘Mtoni Palace Ruins’ na kupata maelezo ya
kihistoria na hatimae alipata mapumziko yalioambatana na burudani mwanana
kutoka kikundi cha Rahatul-zaman na kutumbuizwa kwa nyimbo zilizoibwa na
Kitukuu cha Siti Bint Saada pamoja na mpiga Ganon maarufu Zanzibar Nasor Mohamed hapo katika
mkahawa wa hoteli hiyo.
Katika ziara yake hiyo, Dk.
Shein alifuatana na viongozi mbali mbali wa vyama na Serikali
Comments
Post a Comment