VIONGOZI WA AMCOS 10 ZILIZOHUJUMU MINADA YA KOROSHO PWANI WATIWE MBARONI-RC NDIKILO Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoani Pwani, ambae pia ni mkuu wa Mkoa huo, mhandisi Evarist Ndikilo ,akionyesha picha zinazoonyesha korosho zilizochanganywa mawe na mchanga ,na kusababisha kutia doa minada ya Korosho inayoendelea mkoani hapo ,wakati alipokuwa wilayani Mkuranga. Na Mwamvua Mwinyi,Mkuranga MWENYEKITI wa kamati ya ulinzi na usalama mkoani Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo ameliagiza jeshi la polisi mkoani hapo ,kuwakamatana na kuwahoji viongozi wa vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS)kumi ,kutokana na kosa la kufanya udanganyifu wa ubora na uzito wa korosho ili kujipatia fedha . Amesema kuna baadhi ya AMCOS zimehusika kuchakachua na kutelemsha ubora wa korosho pamoja na kuweka mawe na michanga kwenye magunia ya korosho zilizokuwa zinauzwa kwenye minada . Aidha mhandisi Ndikilo ,amekemea maghala ya vichochoroni na majumbani ambayo yamejaa na kusaba...