Posts

TANZANIA KUNUFAIKA NA BILIONI 120/- KUTOKA GEF KULINDA MAZINGIRA

Image
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga akifungua Warsha ya siku mbili ya Wadau na Wataalamu wa Mazingira inayolenga kuainisha vipaumbele vya miradi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi inayosimamiwa na GEF jijini Dodoma  Februari 13, 2023. Wadau na Wataalamu wa Mazingira wakiwa katika Warsha inayolenga kuainisha vipaumbele vya miradi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi inayosimamiwa na GEF jijini Dodoma Februari 13, 2023. Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga (kulia) akiteta Mwakilishi wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) anayeshughulikia Mfuko wa GEF, Bi. Christine Haffner-Sifakis (kushoto) wakati kifungua Warsha ya siku mbili ya Wadau na Wataalamu wa Mazingira inayolenga kuainisha vipaumbele vya miradi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi inayosimamiwa na GEF jijini Dodoma leo Februari 13, 2023. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Switbert Mkama Mgeni rasmi Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais ...

RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DK.HUSSEIN ALI MWINYI AFUNGUA MAONESHO YA SIKU 3 YA UTALII NA UWEKEZAJI ZANZIBAR 2023

Image
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imedhamiria kwa dhati kuiendeleza sekta ya Utalii na kuongeza thamani na ubora kwa kutumia mikakati tofauti ikiwemo kuongeza vivutio. Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo alipofungua Maonesho ya siku 3 ya Utalii na Uwekezaji Zanzibar 2023 yenye washiriki zaidi ya 200 kutoka Mataifa mbalimbali duniani.  Maonesho hayo yenye maudhui ya 'Greener Zanzibar'  ambayo yanalenga kuibadilisha  Zanzibar kuwa fikio la utalii endelevu, yaani 'Sustainable Tourism Destination' 📅 09 Februari 2023, 📍 Jengo la Kihistoria la Beit El Amaan, Zanzibar

RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DK.HUSSEIN ALI MWINYI AMEKUTANA NA MKURUGENZI MKAZI WA BENKI YA DUNIA NCHINI TANZANIA NATHAN BELETE NA UJUMBE WAKE

Image
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amekutana na Mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Nathan Belete na ujumbe wake.    Dk. Mwinyi ameipongeza Benki hiyo inavyoiunga mkono Zanzibar katika Miradi mikubwa hasa mradi wa Umeme, Afya na Elimu.   Rais Dk.Mwinyi ameiomba benki ya Dunia kusaidia katika Elimu ya Ufundi hasa kutokana na Wanafunzi wengi kutopata nafasi ya vyuo vikuu.   Dk.Mwinyi amemueleza Mkurugenzi huyo sera ya uchumi wa Zanzibar ni Uchumi wa Buluu, Utalii na Bandari, pia katika suala la miundombinu Serikali imekamilisha ujenzi wa uwanja wa ndege wa Kimataifa Unguja na sasa nguvu zimeelekezwa kujenga uwanja mpya wa ndege wa Kimataifa wa Pemba.    Pia, Dk.Mwinyi aliitaka benki hiyo kuharakisha mchakato wa upatikanaji wa fedha za miradi ya maendeleo  08 Februari 2023   📍 Ikulu ,Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi atembelewa na Madaktari wapya kutoka China wakiongozwa na Balozi mdogo wa China, Zanzibar Mhe. Zhang Zhisheng

Image
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema ujio wa madaktari bingwa kutoka China ni fursa adhimu kuimarisha sekta ya Afya Zanzibar.   Dk. Mwinyi amesema timu ya madaktari bingwa kutoka China imewasili Zanzibar kuongeza nguvu katika sekta ya Afya kwa kutoa wataalamu mbalimbali wakiwemo Madaktari bingwa wa operesheni bila kupasua, magonjwa ya kina mama, magonjwa ya meno, magonjwa ya koo, macho na masikio pamoja na kutoa vifaa vya kisasa.     Madaktari hao watafanya kazi za kitabibu katika hospitali za Mikoa ya Unguja na Pemba ikiwemo Hospitali ya Mnazi Mmoja, Abdalla Mzee, Chake Chake na Kivunge.   Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo alipotembelewa Ikulu Zanzibar na Madaktari wapya kutoka China    Ujumbe huo wa Madaktari umeongozwa na Balozi mdogo wa China, Zanzibar Mhe. Zhang Zhisheng     📅 08 Februari 2023   📍 Ikulu ,Zanzibar.

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKIONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI KILICHOFANYIKA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.

Image
 

SIASA ZA KIISTARABU ZA RAISI SAMIA NA KUMBUKUMBU YA TUKIO LA " DINNER TABLE BARGAIN 1790 " NCHINI MAREKANI

Image
Ilikuwa Usiku Wa June 20, 1790 Wakati Mikutano Ya " Congress " Inafanyika Jijini Newyork .Thomas Jefferson Wakati Huo Akiwa Secretary Of The State( Baadae Raisi Wa Tatu Wa Marekani) Alipoamua Kuwaalika Chakula Cha Usiku Watu Wawili Alexander Hamilton Wakati Huo Akiwa Secretary Of Treasure  Na James Madison Mwakilishi Wa Jimbo La Virginia( Baadae Raisi Wa Nne Wa Marekani). Ni Majadiliani Katika Kikao Hiki "Dinner Table Bargain Of 1790" Kilichoitishwa Na Jafferson Ndicho Kilicholeta Suluhu Hasa Baada Ya Madison Kukubali Hoja Ya Hamilton Na Kushawishi Majimbo Ya Kusini Kuunga Mkono Hoja Na Kwa Pamoja Kulijenga Taifa Lao Ambalo Leo Ni Moja Ya Mataifa Makubwa Na Yenye Nguvu Duniani. Na Kassim Mpingi  Rufiji-Pwani  Bila Shaka Taifa Linaunganishwa Na Siasa Za Umoja,Mshikamano,Kusameheana Na Kujenga Nchi Kwa Pamoja(4R). Vyama Pinzani Baada Miaka Saba Vinaingia Tena Mtaani Kufanya Mikutano Na Kufurahi Matunda Ya Siasa  Safi Na Za Kiistarabu Za Raisi Samia . Aina Hii Ya Siasa...

HOSPITALI YA KISASA KITOGANI,WILAYA YA KUSINI UNGUJA YAFUNGULIWA NA RAIS MWINYI

Image
 Na Mwandishi wetu Zanzibar Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi afungua Hospitali ya  Kisasa ya Kitogani Wilaya ya Kusini  ,Mkoa wa Kusini Unguja. Kufunguliwa kwa Hospitali hii  pia imeambatana na kufungwa kwa  Vifaa tiba vipya,Gari la kubebea wagonjwa,hospitali ipo tayari kutoa huduma tofauti,ikiwemo huduma za wagonjwa wa nje(OPD),Mama na Mtoto ,huduma za kliniki mbalimbali zikiwemo za Pua,Koo,Masikio ,Macho,Magonjwa yasio ya kuambukiza kama Sukari,shinikizo la damu ,huduma za madawa(pharmacy),huduma za Wagonjwa wanaolazwa ikiwemo ,Wodi za Watoto,Mama Wajawazito kabla na baada ya kujifungua,Watu wazima Wanawake na Wanaume,huduma za wagonjwa wa dharura na ajali,Wagonjwa mahututi(ICU),huduma za watoto njiti ,Wodi tatu za wagonjwa wenye mahitaji maalum ya  kujitenga(isolation) pia Kuna Theatres mbili (2)za kisasa, huduma za ushauri nasaha na kupiga vita vitendo vya udhalilishaji na huduma za uchunguzi ikiwemo Maaba...