RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DK.HUSSEIN ALI MWINYI AMEKUTANA NA MKURUGENZI MKAZI WA BENKI YA DUNIA NCHINI TANZANIA NATHAN BELETE NA UJUMBE WAKE








 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amekutana na Mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Nathan Belete na ujumbe wake. 

 

Dk. Mwinyi ameipongeza Benki hiyo inavyoiunga mkono Zanzibar katika Miradi mikubwa hasa mradi wa Umeme, Afya na Elimu.

 

Rais Dk.Mwinyi ameiomba benki ya Dunia kusaidia katika Elimu ya Ufundi hasa kutokana na Wanafunzi wengi kutopata nafasi ya vyuo vikuu.

 

Dk.Mwinyi amemueleza Mkurugenzi huyo sera ya uchumi wa Zanzibar ni Uchumi wa Buluu, Utalii na Bandari, pia katika suala la miundombinu Serikali imekamilisha ujenzi wa uwanja wa ndege wa Kimataifa Unguja na sasa nguvu zimeelekezwa kujenga uwanja mpya wa ndege wa Kimataifa wa Pemba. 

 

Pia, Dk.Mwinyi aliitaka benki hiyo kuharakisha mchakato wa upatikanaji wa fedha za miradi ya maendeleo

 08 Februari 2023

 

📍 Ikulu ,Zanzibar.

Comments

Popular posts from this blog

JUHUDI ZA MWALIMU NYERERE KATIKA KUKUZA NA KUIMARISHA SEKTA YA UTALII NCHINI