Mkurugenzi wa Uratibu Shuhuli za Serikali kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Ndg.Khalid Bakari Amran, akimuonyesha tuta linalojengwa na kaya masikini shehia ya ndagoni lenye urefu wa mita 200, Naibu waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe:Mihayo Juma N’hunga,  wa pili kutoka kulia wakati alipotembelea kukagua kazi zinavyoendelea katika tuta hilo
Hili  tuta linalojengwa kwa ajili ya kuzuwia maji Chumvi lenye urefu wa mita 200, linalojengwa kwa nguvu kazi za wanakaya katika bonde la Kidau shehia ya Ndagoni, baada ya kumalizika ujenzi wake litaweza kuwarudisha wakulima zaidi ya 300, kuendelea kulima katika mashamba yao baada ya kuyahama kwa zaidi ya miaka miwili sasa
Mratibu wa Tasaf Pemba Ndg.Mussa Said, akitoa maelezo ya ujenzi wa Tuta la kuzuwia maji ya Chumvi lenye urefu wa mita 200, kwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe:Mihayo Juma N’hunga, wakati alipotembelea wanakaya wa shehia ya Ndagoni
Zaidi ya wakulima 300 waliokuwa wakilima mpunga katika bonde la Kidau, wameshindwa kufanya shuhuli zao za kilimo baada ya bonde hilo kuingia maji Chumvi, ambapo sasa mradi wa kunusuru kaya masikini unaendelea na ujenzi wa tuta lenye urefu wa mita 200 katika bonde hilo
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mhe:Mihayo Juma N’hunga, akizungumza na walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini Shehia ya Ndagoni Kisiwnai Pemba, katika ziara yake ya siku mbili kisiwani hapa, kuangalia miradi mbali mbali ya maendeleo inayotekelezwa na Tasaf Pemba
Mkurugenzi wa Uratibu Shughuli za Serikali kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Khalid Bakari Amran, akizungumza na wanakaya masikini shehia ya Ndagoni Wilaya ya Chake Chake, mara baada ya kukagua kazi za ujenzi wa tuta lakuzuwia maji Chumvi
Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Pemba Mhe:Salama Mbraouk Khatib, akizungumza na walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini Shehia ya Ndagoni, huko katika bonde la Kidau mara baada ya kumaliza kazi ya ujenzi wa tuta la kuzuwia maji chumvi
Mratibu wa Tasaf Pemba Ndg.Mussa Sadi Kisenge, akitoa ufafanuzi ya fedha kwa wanakaya masikini shehia ya ndagoni, juu ya ujenzi wa tuta lenye urefu wa mita 200 katika bonde la Kidau kwa lengo la kuzuwia maji chumvi
Viongozi mbali mbali wa Serikali wakiongozwa na Naibu waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Mhe:Mihayo Juma N’hunga wapili kutoka kushoto, Mkurugenzi wa Uratibu kutoka ofisi hiyo Zanzibar Mhe;Khalid Bakar Amran, Mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Mhe:Salama Mbarouk Khatib, Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamu wa Pili Salum Ali Matta na katibu Tawala Wilaya ya Chake Chake Abdalla Rashid.
(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.

Comments

Popular posts from this blog

JUHUDI ZA MWALIMU NYERERE KATIKA KUKUZA NA KUIMARISHA SEKTA YA UTALII NCHINI