Kamati ya GFT yakagua maendeleo ya Mradi wa JNHPP, yaipongeza serikali

Kamati ya Uwezeshaji ya Mradi wa kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali (GFT) imeipongeza serikali kwa kupiga hatua zaidi katika utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo.

Pongezi hizo zimetolewa na Meneja Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TAZARA) Mhandisi Fuad Abdallah kwa niaba ya wajumbe wote wa GFT wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi huo inayofanyika katika maeneo tofauti ya mradi huo, kuanzia June 6-11, mkoani Pwani. 

Mhandisi Fuad alisema kuwa wamefanya ziara hiyo kwa kukagua maeneo mbalimbali ya mradi huo ambapo walikagua maendeleo ya ujenzi wa Tuta kuu la Bwawa, Kituo cha Kuchochea Umeme, Nyumba ya kuendeshea Mitambo ya kuzalisha umeme na Kingo za Bwawa (Saddle Dam)

Muonekano wa eneo la kupeleka maji katika mitambo ya kufua umeme katika mradi wa JNHPP, Wajumbe wa Kamati ya Uwezeshaji ya Mradi wa kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali (GFT)walifa nya ziara ya kukaua eneo hilo June 6-8, 2022 mkoani Pwani

Muonekano na Tuta kuu la bwawa la kufua umeme, Wajumbe wa Kamati ya Uwezeshaji ya Mradi wa kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali (GFT) walifanya ziara ya kukagua eneo hilo June 6-8, 2022 mkoani Pwani.

Wajumbe wa Kamati ya Uwezeshaji ya Mradi wa kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali (GFT) wakiwa katika majadiliano baada ya kufaya ziara ya kukagua mradi huo, iliyofanyika June 6-8, 2022, Mkoani Pwani.



Mwenyekiti wa Kamati ya uwezeshaji ya Mradi wa Julius Nyerere(JNHPP, kutoka Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali(GFT) ambaye pia ni Mratibu wa mradi huo kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Christopher Bitesigirwe akizungumza na wajumbe wa Kamati hiyo wakati mkutano, baada ya ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo iliyofanyika Juni 6-8, 2022, mkoani Pwani.




Comments

Popular posts from this blog

JUHUDI ZA MWALIMU NYERERE KATIKA KUKUZA NA KUIMARISHA SEKTA YA UTALII NCHINI